Museveni aketi barabarani kupokea simu
Je ushawahi kupokea simu ya dharura? Je wewe hujitenga vipi na watu waliokaribu nawe ima ni mkeo ama hata wafanyakazi wenza ili upokee simu ya kibinafsi?
 |
Museveni alipokea simu kando ya barabara wilaya ya Isingiro, karibu na mpaka wa Uganda na Tanzania |
Amini usiamini Rais Yoweri Museveni, alishuka kutoka kwenye gari lake rasmi akachukua kiti chake na kukiweka kando kando ya barabara mpya ya Isingiro ikipitia kijiji hicho cha Kyeirumba hadi Tanzania na kupokea simu faraghani.
Mzee Museveni kama vile baba wa taifa alitumia muda wake kufanya shughuli hiyo huku akiwapungia mkono wapita njia.
Baada ya dakika 30 hivi raia wa kijiji hicho walishangaa kuwa miongoni mwa maafisa wakuu serikalini.
Wengine wanamkejeli kwa kuhofia kudukuliwa huku wengine wakimkosoaa kwa kuketi barabarani.
''Kwani hangeweza kupokea simu yake ndani ya gari lake?"
''Ni siri gani hiyo ambayo hakutaka hata walinzi wake wasikie.
''Ama ilikuwa ni #Besigyexit?", wakizungumzia kuachiliwa kwa dhamana kwa kiongozi wa upinzani Dkt Kizza Besigye mapema asubuhi.
Post a Comment