[6] [recent] [slider-top-big] [Music]
You are here: Home / Askofu Gwajima amjibu Katibu Mkuu CCM aliyemuita muongo

Askofu Gwajima amjibu Katibu Mkuu CCM aliyemuita muongo

| No comment


Askofu wa kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima inaelezwa kuwa amemjibu Katibu Mkuu mstaafu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kufuatia kauli yake aliyoitoa Dodoma Julai 23 kuwa Gwajima ni muongo kwa kuwa alisema Rais Jakaya Kikwete hakuwa akitaka kukabidhi kiti cha uenyekiti kwa Rais Magufuli kitu ambacho si kweli.
Akihubiri jana kanisani kwake, Askofu Gwajima alisikika akisema maneno ambayo yalionekana kumlenga Katibu Mkuu huyo mstaafu, Yusuf Makamba licha ya kuwa hakumtaja jina, alisema kuwa Leseni yake yeye ni ya kuendesha magari makubwa na siyo vibajaji na maguta.
Siwezi kushughulika na vigari vidogo vidogo, nyie mnajua leseni yangu ni ya kuendesha semi trailer, alisema Gwajima wakati wa mahubiri kanisani kwake.
Gwajima amekuwa akikabiliwa na tuhuma za uchocheza na siku za hivi karibuni alikamatwa uwanja wa ndege wa Julius Nyerere na kuhojiwa na polisi kwa maneno yake ya uchochezi aliyoyatoa kuhusu serikali.